HABARI MPYA

Home Top Ad

Post Top Ad

Friday, February 5, 2016

HALMASHAURI JIJI KUJA NA MRADI WA UBORESHAJI MJI (SMART AREA)

 Mkuu wa Itifaki na Mawasiliano wa Jiji la Dar es Salaam Gaston Makwembe, akizungumza na wandishi wa habari (hawapo picha)  leo jijini Dar es Salaam, juu ya mradi wa kuboresha jiji unagharimu sh.milioni 500 ambao unatarajia kuanza Julai Mwaka huu,kulia ni Mkuu wa Idara ya Udhibiti Taka Protus Membe. 
Wandishi wahaba habari wakimsikiriza Mkuu wa Itifaki na Mawasiliano wa Jiji la Dar es Salaam Gaston Makwembe.
(Picha na Emmanue Massaka wa Globul ya Jamii)

Na Chalila Kibuda,Globu ya Jamii
HALMASHAURI ya Jijin la Dar es Salaam kutengeneza jiji katika ubora (Smart Area) ikiwamo kuondoa biashara zisizo rasmi katikati ya jiji.

Akizungumza na waandishi wa habari leo,Mkuu wa Itifaki na Mawasiliano wa Jiji, Gaston Makwembe amesema kuwa mradi huo wa kuboresha jiji unagharimu sh.milioni 500 ambao unatarajia kuanza Julai Mwaka huu.

Makwembe amesema katika uboreshaji huo utakwenda sambasamba na uondoaji wa ombaomba katika ya jiji la Dar es Salaam.

Maeneo yatakayoguswa ni barabara ya Kawawa kutoka makutano ya Kawawa na Karume hadi makutano ya Kawawa na Ali Hassan Mwinyi ,Makutano ya Mandela na Pungu pamoja maeneo ya mjini na Uwanja wa Ndege.


Makwembe amesema katika uboreshaji huo ni pamoja na uzuiaji wa Pikipiki,bajaji,Maguta pamoja na gari zinazozidi tani 10 kuingia katikati ya jiji.

No comments:

Post a Comment

Post Bottom Ad