Mzee wa mtaa kwa mtaa blog katika kuhakikisha libeneke lako pendwa halilali njaa moja kwa moja mpaka eneo la Tunduma wilayani Momba mkoani Mbeya na kukuta haya mashimo yakiwa kwa wingi kuanzia eneo la kilimanjaro mpaka eneo la Ccm Tunduma, binafsi nimeshindwa kuelewa kwani hii ndio fasheni ya barabara kuu huku au hayajaonwa haya mashimo yaliyopo huku maana hii ndio barabara kuu tena hutumika na watu wengi kutoka sehemu mbalimbali na ukizingatia huku ni mpakani na mji umechangamka kwa kuwa na watu wengi sasa kwa barabara hii kweli tutafika?
Ona mashimo jinsi yalivyo kuwa makubwa na hii ni kero kwa watumiaji wabarabara hiyo ikiwemo madereva wa magari,bajaji, pikipiki hata baiskeli
wahusika wa hili tuliangalie hili tusilifumbie macho kwani hii ni hatari
na Fadhiri Atick Mbeya.
No comments:
Post a Comment