Mkuu wa wilaya ya Makete Josephine Matiro ametoa agizo kwa uongozi wa kata ya Matamba kufanya mikutano ya kuwaelewesha wananchi umuhimu wa kujenga nyumba zao katika hali ya uimara pamoja na kupanda miti ya matunda pembezoni mwa nyumba zao
Ametoa agizo hilo hivi karibuni wakati alipotembelea eneo lililopata maafa ya kuezuliwa nyumba na upepo mkali ulioambatana na mvua na kugundua kuwa ujenzi hafifu wa nyumba zao nao umechangia kwa kiasi kikubwa hasara hiyo
"Wananchi wanajenga nyumba hazina makoa, maeneo ni wazi hayana miti achilia mbali ya matunda lakini hata mingine hakuna, haya maafa hayataisha, mtendaji nakuagiza ufanye mikutano na wananchi na taarifa nipewe" alisema Matiro
katika tukio hilo hakuna vifo wala majeruhi ya watu, zaidi ya nyumba na baadhi ya vitu vilivyokuwa ndani kuharibika
Moja
ya Nyumba ya mkazi wa kijiji cha Nungu kilichopo kata ya Matamba
wilayani Makete iliyoezuliwa na upepo mkali ulioambatana na mvua hivi
karibuni, hakuna mtu aliyefariki wala kujeruhiwa kutokana na hali hiyo
Mkuu
wa wilaya ya Makete Mh. Josephine Matiro (kulia) akiangalia moja ya
nyumba iliyobomoka kutokana na upepo huo mkali, kulia kwake ni baadhi ya
wajumbe wa kamati ya ulinzi na usalama ya wilaya ya Makete.
Nyumba iliyobomolewa na mvua na upepo mkali
Mkuu wa wilaya akiangalia nyumba ya mkazi mwingine iliyoharibika
Mkuu wa wilaya ya Makete akitoa maagizo baada ya kujionea hali halisi eneo la tukio
Mkuu
wa wilaya ya Makete Josephine Matiro (kushoto) akiwa na baadhi ya
wajumbe wa kamati ya ulinzi na usalama wilaya ya Makete wakisiliziza
jambo eneo la tukio.
Afisa
mtendaji wa kijiji cha Nungu Bw. Ngogo akitoa taarifa mbele ya kamati
ya ulinzi na usalama kuhusu tukio hilo (Picha zote na Edwin Moshi wa
Eddy Blog)
No comments:
Post a Comment