HABARI MPYA

Home Top Ad

Post Top Ad

Thursday, December 18, 2014

MFUKO WA AFYA YA JAMII WATOA MAFUNZO KWA WAJASILIAMALI KUHUSU BIMA YA AFYA

Na Bakari Issa,Dar es Salaaam

Wajasiriamali toka vikundi mbalimbali wamehamasishwa kujiunga na Mfuko wa Taifa wa Bima ya Afya (NHIF) ili kurahisisha matibabu wawapo katika shughuli zao za kawaida,leo katika ukumbi wa Msimbazi Centre jijini Dar es Salaam.

Katika Mpango mpya uliozinduliwa na Mfuko huo ujulikanao kama Mpango wa Kikoa(MATUAL PLAN),Wajasiriamali watakaojiunga na mfuko huo na kuwa wanachama watalipia shilingi 76,800 kwa mwaka ili kupata matibabu kupitia mfuko huo.

Akizungumza na wajasiriamali kutoka vikundi mbalimbali ambavyo vipo chini ya Muungano wa vikundi mbalimbali vya kuinua jamii(ASE),Mkurugenzi wa Mfuko wa Afya ya Jamii kutoka Mfuko wa Bima ya Afya,Rehani Athumani amewataka wajasiliamali wanaofanya biashara ndogondogo wasione ngumu kujiunga na Mfuko huo wa Bima ya Afya na amewataka viongozi kuwa na ushirikiano wanapopata matatizo na changamoto katika kufanikisha suala hilo.

“Wajasiriamali wa biashara ndogondogo nawashauru kujiunga na mfuko huu,na nawasihi viongozi wenzangu kuwa na ushirikiano tunapopatwa na matatizo pamoja na changamoto”,alisema Rehani.

Kwa upande wake,Afisa Matekelezo na Uratibu(NHIF),Catherine Masingisa amesema kuwa mpango huo ni kwa wote,watoto na wakubwa kwa mjasiriamali kuchangia mfuko huo wa Bima ya Afya,hata hivyo amesema mpango huo utakuwa na matibabu sawa na ule mpango wa Watumishi wa Serikali.

“Mpango huu wa Kikoa ni utaratibu wa kupata huduma ya afya kwa wajasiriamali wadogowadogo katika vikundi na wanachama watapata huduma ya matibabu kwa unafuu zaidi na kuondoa kabisa suala la unyanyasaji kwa wajasiriamali”,alisema Catherine.

Naye,Mratibu Mkuu wa ASE,Bi.Sunayritha Mapunda amewataka wajasiriamali hao walioko katika muungano huo wa vikundi mbalimbali vya kuinua jamii kuonyesha mfano kwa wajasiriamali wengine walioko nchini kujiunga na Mfuko huo wa Taifa wa Bima ya Afya.
 Mkurugenzi wa Mfuko wa Afya ya Jamii (CHF), Rehani Athumani akiongea na vikundi mbalimabli vya wajasiliamali kuhusu umuhimu wa mfuko wa Afya ya jamii pamoja na kuwahamasisha wajasiliamali hao kufungua bima ya afya kwa ajili ya matibabu.
Mratibu wa Mtandao wa Mfuko wa Afya ya Jamii(TNCHF), Camillius Mathew Haule akitoa maelekezo juu ya ujazaji wa fomu za Mfuko wa Afya ya Jamii kwa wajasiliamali hao
Afisa Matekelezo na Uratibu wa Mfuko wa Taifa wa Bima ya Afya (NHIF) Catherine Masingisa akizungumza na wajasiliamali juu ya mfuko wa afya unavyofanya kazi hapa nchini.
Mratibu wa Mtandao wa Mfuko wa Afya ya Jamii (TNCHF), Kidani Mhenga akitoa elimu kwa wajasiliamali hao
Afisa Matekelezo na Uratibu wa Mfuko wa Taifa wa Bima ya Afya (NHIF), Salvatory F. Okumu akieleza juu ya kadi ya bima ya afya kwa wajasiliamali waliofika kwenye mafunzo hayo.
Mjasiliamali Bi. Tipwa Mapunda akichangia mada
Afisa Matekelezo na Uratibu wa Mfuko wa Taifa wa Bima ya Afya (NHIF), Salvatory F. Okumu(wa kwanza kushoto) akimkabidhi Bi. Sunayritha Simon Mapunda fomu ya usajili kwa ajili ya kujiunga na mfuko wa Afya ya Jamii.na katikati ni Mratibu wa Mtandao wa Mfuko wa Afya ya Jamii (TNCHF), Kidani Mhenga
Bi. Sunayritha Simon Mapunda akionesha fomu ya mfuko wa Afya ya Jamii kwa wajasiliamali (hawapo pichani) waliofika kwenye mafunzo hayo
Baadhi ya wajasiliamali waliofika kwenye mafunzo hayo

No comments:

Post a Comment

Post Bottom Ad