HABARI MPYA

Home Top Ad

Post Top Ad

Thursday, November 20, 2014

ZIFF KUPOKEA FILAMU KWA NJIA YA TOVUTI

Tamasha la Filamu la Nchi za Jahazi (ZIFF) limekuwa tamasha la kwanza Afrika kukubali filamu zitumwe kupitia mtandao. Filamu hizo zitakazoshindanishwa, sasa zitalipiwa fedha kidogo wakati zikitumwa.

Kwa sababu ya kukua kwa mtandao wa dunia, matamasha mengi sasa yanapokea filamu mtandaoni ili kuweza kuanza kuzitazama filamu hata kabla muda wa kutuma filamu haujaisha, kama ilivyokua zamani. Kwa njia hiyo wachaguaji filamu wanapata muda mrefu zaidi wa kuzitazama filamu kwa kituo.

ZIFF sasa haitaikubali filamu toka nchi za nje kama haikutumwa kupitia mtandao. Hata hivyo Watanzania watapewa upendeleo na kuruhusiwa kutuma filamu zao kama zamani na pia hawana haja ya kulipa karo ya Euro 5 ambazo wengine watalipia.

“ZIFF imesaini mkataba na FESTHOME, shirika lenye jukwaa la kimataifa la upokeaji wa filamu kwa mashindano”, alisema Daniel Nyalusi, Meneja wa Tamasha la ZIFF na kuongeza, “ Kusema kweli hii inawapunguzia watengeneza filamu hata gharama za utumaji filamu. Kwa kuzituma mtandaoni tutahakikisha kazi inafanyika haraka na kuwajulisha wateja mapema kuhusu filamu zao”.

Watu wataweza kutuma mafaili ya Vimeo yenye hadhi ya MP4 au mfumo wowote mwingine.

ZIFF ni jukwaa muhimu linalowezesha wadau wa filamu kuonyesha filamu zao na zikapimwa kimataifa. Tamasha la ZIFF bado linadhaminiwa na Kampuni ya ZUKU na litafanyika Zanzibar kuanzia tarehe 18 hadi 26 Julai 2015. Mwisho wa kupokea filamu ni Tarehe 31 Januari, 2015 hii ni pamoja na Bongo Movie.

No comments:

Post a Comment

Post Bottom Ad