Itakumbukwa katika mkutano uliofanyika mapema mwezi huu jijini "CAIRO" hofu ya ukuwaji wa uhalifu mtandao unaoweza kurudisha nyuma uchumi wa mataifa ya Afrika ulipata kujadiliwa kwa kina huku nchi ya Misri ikionyesha washiriki wa mkutano huo jitihada inayoendelea nayo katika kukabiliana na uhalifu mtandao.
Ime ripotiwa na Mtandao wa "MGAFRICA" kuhusiana na kilichojiri katika mkutano uliokamilika jijini Johannesburg, Afrika kusini wa maswala ya usalama mitandao ambapo Bara la Afrika limetabiriwa kuwa na ukuaji wa uhalifu mtandao kutokana na mikakati daifu ya kujiweka salama huku ikiwapatia wahalifu mtandao urahisi mkubwa wa kuleta maafa siku za usoni.
Kumeendelea kuwa na wimbi kubwa la uhalifu mitandao ingawa jitihada za kukabiliana na uhalifu huo zimeendelea kugharimu mataifa mengi hivi sasa. Mataifa yamekua yakiwekeza kwenye maswala ya usalama mitandao lakini bado wahalifu mtandao wameonekana kuendelea kutamba.
Mkutano huo wa maswala ya usalama mitandao uliangazia kwa karibu sababu za ukuaji wa uhalifu mtandao na nini kifanyike kwa mataifa ili kuweza kupiga hatua ya kubaki salama kimtandao. Wataalam wa maswala Mtandao kutoka katika mataifa mbali mbali walikutana kuyajadili mambo hayo kama ifuatavyo: BOFYAHAPA
No comments:
Post a Comment