HABARI MPYA

Home Top Ad

Post Top Ad

Friday, October 24, 2014

MOI yajiimarisha katika utoaji huduma muhimu za Tiba na Upasuaji

Na Hassan Silayo-MAELEZO

Taasisi ya Tiba ya Mifupa, Upasuaji wa Ubongo na Mishipa ya Fahamu (MOI) imeendelea kuwa nguzo muhimu nchini katika utoaji wa huduma za tiba na upasuaji.

Hayo yamesemwa na Afisa Uhusiano wa Taasisi hiyo Bw. Patrick Mvungi wakati wa Mkutano na waandishi wa habari leo Jijini Dar es Salaam.

Patrick amesema kuwa MOI imesaidia kuokoa zaidi ya asilimia 95 ya watanzania ambao kwa namna moja au nyingine wangeweza kupoteza maisha yao au kupata ulemavu wa kudumu kutokana na ajali.

“MOI kwa kiasi kikubwa imefanikiwa kuokoa maisha ya watanzania kwa zaidi ya asilimia 95 kutokana na kutoa huduma muhimu ya za tiba na upasuaji wa wagonjwa wanaopokelewa na hivyo kupunguza vifo na rufaa za kuwapeleka wagonjwa nje ya nchi” alisema Mvungi.

Akizungumzia kuhusu upasuaji wa kitaalam wa mgongo (specialized Spine Surgeries) Mvungi alisema kuwa Taasisi hiyo imeendelea kufanya na zaidi ya asilimia 99 ya wagonjwa waliofanyiwa upasuaji wamepona na kurudi katika hali zao za kawaida.

Naye Meneja Ustawi wa Jamii na Uhusiano wa Taasisi Taasisi hiyo Bw. Almas Jumaa alisema kuwa zaidi ya wagonjwa 1,256 ya wagonjwa wa upasuaji mkubwa wa nyonga walipasuliwa salama na zaidi ya asilimia 95 ya wagonjwa hao wamepona kabisa.

Pia Almas alisema kuwa pia Taasisi imeendelea kutoa matibabu ya magonjwa ya ubongo yaliyokuwa yanahitaji upasuaji yamefanikiwa kufanyika kwa zaidi ya asilimia 80 na wagonjwa waliokuwa na matatizo hayo wamepona na kuondolewa kwenye hatari ya kupoteza uhai.

Taasisi ya MOI imewataka watanzania kuitumia Taasisi hiyo na kuacha kufuata matibabu nje ya nchi kwa gharama kubwa tofauti na kama wangepata huduma hizo hapa nchini kwa gharama nafuu.
Afisa Uhusiano wa Taasisi ya Tiba ya Mifupa, Upasuaji wa Ubongo na Mishipa ya Fahamu (MOI) Bw. Patrick Mvungi akieleza kwa vyombo vya habari(hawapo pichani) kuhusu mafanikio ya Taasisi hiyo ikiwemo kufanikiwa kwa zaidi ya asilimia 95 ya kutoa huduma muhimu za Tiba na Upasuaji kwa wagonjwa wanaopokelewa na hivyo kupunguza vifo na rufaa za kuwapeleka wagonjwa nje ya nchi,wakati wa mkutano uliofanyika leo Jijini Dar ea Salaam. Kushoto ni Meneja Ustawi wa Jamii na Uhusiano wa Taasisi hiyo Bw. Almas Jumaa.
Meneja Ustawi wa Jamii na Uhusiano wa Taasisi ya Tiba ya Mifupa, Upasuaji wa Ubongo na Mishipa ya Fahamu (MOI) Bw. Almas Jumaa akiwaeleza waandishi wa habari (hawapo pichani) jinsi Taasisi hiyo ilivyoendelea kuwa nguzo Muhimu katika kuokoa maisha ya watanzania ambapo upasuaji wa kitaalam wa mgongo umeendelea kufanyika na kufanikiwa kwa zaidi ya asilimia 99 na kusaidia kuwaondoa wagonjwa wenye tatizo hilo katika hatari ya kupotea uhai.Kulia ni Afisa Uhusiano wa Taasisi hiyo Bw. Patrick Mvungi. PICHA NA MAELEZO.

No comments:

Post a Comment

Post Bottom Ad