HABARI MPYA

Home Top Ad

Post Top Ad

Saturday, August 30, 2014

Bodi ya ya Wakurugenzi ya Mamlaka ya Maji Safi na Maji Taka Dar es Salaam (DAWASA) yatembelea Eneo la Mradi wa Ujenzi wa Bwawa la Maji Kidunda

Meneja Usimamizi, Uendeshaji na Mazingira toka Mamlaka ya Maji Safi na Maji Taka Dar es Salaam (DAWASA) Bi.Modesta Mushi akiwaonesha wajumbe wa Bodi ya Wakurugenzi ya Mamlaka ya Maji Safi na Maji Taka Dar es Salaam (DAWASA) ramani ya maeneo yatakayoguswa na Ujenzi wa Mradi wa Bwawa la Kidunda lenye ujazo wa Mita milioni 190, wakati wa Ziara ya Bodi hiyo katika eneo la Mradi Mkoani Morogoro.
Mkuu wa Msafara wa Timu ya Ulipaji fidia kwa Wakazi walio katika Eneo la Mradi Mhandisi John Kirecha akitoa maelezo kwa Wajumbe wa Bodi ya Wakurugenzi ya Mamlaka ya Maji Safi na Maji Taka Dar es Salaam (DAWASA) (Hawapo pichani)kuhusu kukamilika kwa taratibu za ulipaji fidia kwa wakazi waliopisha ujenzi wa mradi wa bwana la Kidunda litakaloweza kutoka huduma kwa mikoa ya Dar es Salaam, Pwani na Morogoro, wakati wa Ziara ya Bodi hiyo katika eneo la Mradi Mkoani Morogoro.
Makamu Mwenyekiti wa Bodi ya Wakurugenzi ya Mamlaka ya Maji Safi na Maji Taka Dar es Salaam (DAWASA) Alhaji Said El-Maamry akimueleza jambo Mkuu wa Msafara wa Timu ya Ulipaji fidia kwa Wakazi walio katika Eneo la Mradi Mhandisi John Kirecha ikiwemo kuhakikisha taratibu hizo haziathiri maendeleo ya ujenzi wa mradi huo,ikiwamo kuwataka wakazi wenye matatizo ya Mirathi kuyamaliza ndipo waweze kupatiwa fidia zao.

Afisa Mtendaji Mkuu wa Mamlaka ya Maji Safi na Maji Taka Dar es Salaam (DAWASA) Bw. Archard Mtalemwa (katikati mwenye shati jeupe)  akiwaonesha Wajumbe wa Bodi ya Wakurugenzi ya Mamlaka ya Maji Safi na Maji Taka Dar es Salaam (DAWASA) Ramani ya Viwanja 1000 vilivyopimwa  vya Makazi mapya eneo la Bwira juu kwa wakazi 2068 waliopisha Mradi wa  ujenzi wa Bwawa la Kidunda, wakati wa Ziara ya Bodi hiyo katika eneo la Mradi huo Mkoani Morogoro.
Msimamizi wa  Kitengo cha Usimamizi na Upimaji Ramani wa Wilaya Mkoani Morogoro Bw. Kitomaga Francis(aliyevaa Kaunda suti)  akiwaeleza Wajumbe wa Bodi ya Wakurugenzi ya Mamlaka ya Maji Safi na Maji Taka Dar es Salaam (DAWASA) mgawanyiko wa matumizi wa viwanja hivyo ikiwamo kwa ujenzi wa shule, makazi, Hospitali, Polisi, Ofisi na huduma nyingine muhimu za jamii, wakati wa Ziara ya Bodi hiyo katika eneo la Mradi huo Mkoani Morogoro.

Wajumbe wa Bodi ya Wakurugenzi ya Mamlaka ya Maji Safi na Maji Taka Dar es Salaam (DAWASA) wakiondoka eneo la Bwira Juu , eneo lililotegwa kwa ajili ya makazi mapya kwa wananchi waliopisha ujenzi wa Mradi wa Bwawa la Kidunga, wakati wa Ziara ya Bodi hiyo katika eneo la Mradi huo Mkoani Morogoro.(Picha na Hassan Silayo)

No comments:

Post a Comment

Post Bottom Ad