Wednesday, November 25, 2009
Muandishi: Othman Michuzi | Tarehe: Wednesday, November 25, 2009
Marehemu Bernard Japhet Lema enzi za uhai wake

Jumuiya ya wanafunzi wa Hyderabad, India (TSAH) inasikitika kutangaza kifo cha mwanafunzi mwenzao, Bernard Japhet Lema (23) kilichotokea tarehe 24/11/2009 katika hospitali ya Apollo jiji hyderabad. Marehemu alipata ajali ya pikipiki tarehe 21/11/2009 na kukimbizwa hospitali.
Ijapokuwa sisi tulimpenda sana lakini Mungu alimpenda zaidi.
Tunatoa pole kwa familia, ndugu jamaa na marafiki wa marehemu.
Mungu ailaze roho ya marehemu mahali pema.
Amina
 
Tuesday, November 24, 2009
Muandishi: Othman Michuzi | Tarehe: Tuesday, November 24, 2009
maana hii mimi ndio nimeiona kwa mara ya kwanza leo!!!!

Picha na Kaka Maggid Mjengwa.
 
Muandishi: Othman Michuzi | Tarehe: Tuesday, November 24, 2009
jamaa yuko fiti kweli kwenye mambo haya,hebu mcheki alivyo dank hapo.
 
Muandishi: Othman Michuzi | Tarehe: Tuesday, November 24, 2009
Baraza Kuu la Waislamu Tanzania BAKWATA liwametangazia Wislamu na wananchi wote kwamba mwandamo wa mwezi Dhul Hajj umeonekana tarehe 18/11.2009 na kuashiria kuanza kwa mwezi mtukufu wa dhul Hajj (Mfungo Tatu)

Kwa maana hiyo sherehe ya sikukuu ya Eid el Hajj itakuwa mwezi wa 10 Dhul Hajj sawa na Tarehe 28/11/2009.

Sala na Baraza la Idd kitaifa zitafanyika katika msikiti wa Alfarouq uliopo Bakwata Makao Makuu Kinondoni Dar es alaaam , kuanzia saa 1.30 asubuhi na kufuatiwa na Baraza la Idd hadi saa 3.00 asubuhi.

Baraza kuu la Waislamu wa Tanzania BAKWATA linawatakia Eid njema waislamu wote na watanzania kwa ujumla

Imetolewa na
Sheikh Ismail Habib

KAIMU MUFTI WA TANZANIA
 
Monday, November 23, 2009
Muandishi: Othman Michuzi | Tarehe: Monday, November 23, 2009
Mkulima amejiwa na Mwaandishi wa magazeti kumuhoji kuhusu maisha ya shambani. Mkulima huyu hawapendi Waandishi wa habari akaona vyema amchoshe katika kujibu maswali, na mambo yakawa hivi:

MWANDISHI: Wewe unawalisha ng'ombe chakula gani?
MKULIMA: Ng'ombe yupi? Mweupe au Mwekundu?

MWANDISHI: Ng'ombe mweupe.
MKULIMA: Ninamlisha nyasi na viguta vya mahindi.

MWANDISHI: Na mwekundu?
MKULIMA: Vilevile nyasi na viguta vya mahindi.

MWANDISHI: ahaa sawa, na sehemu ya kulala ni wapi?
MKULIMA: Ng'ombe yupi? mweupe au mwekundu?

MWANDISHI: Mweupeee!!!!XXCCCZZZZHH!!!!
MKULIMA: Mweupe ninamlaza bomani kulee...

MWANDISHI: na mwekundu?
MKULIMA: Vile vile namlaza na mwenzie.

MWANDISHI: Hii sehemu yote majumba mengi, wakati wa kulisha unafanyaje?
MKULIMA: Yupi mweupe au mwekundu?

MWANDISHI: Woooteeee!!!! [akifuka kwa hasira]
MKULIMA: Mweupe ninamfunga kamba na kumzungusha malishoni na kumrudisha.

MWANDISHI: na mwekundu vilevile?
MKULIMA: Mwekundu? Mwekundu yeye ninamfunga kamba na kuzunguka nae kama mwenziwe tu.

MWANDISHI: Kwanini kila mara nikikuuliza huduma za ng'ombe wako unaniuliza mweupe au mwekundu halafu inatokea kuwa kazi zao wote ni sawa?????
MKULIMA: Kwa sababu ng'ombe mweupe ni wangu.

MWANDISHI: Na mwekundu?
MKULIMA: Na mwekundu ni wangu vilevile.

shuwaini!
 
Muandishi: Othman Michuzi | Tarehe: Monday, November 23, 2009
 
Muandishi: Othman Michuzi | Tarehe: Monday, November 23, 2009
Mafundi wa mamlaka ya maji safi na maji taka DAWASCO wakizibua chemba ya maji taka kwa kutumia mashine maalum ijulikanayo kama Jeting Machine katika mtaa wa Mkunguni Kariakoo jijini Dar es Salaam.
 
Muandishi: Othman Michuzi | Tarehe: Monday, November 23, 2009

Kitunguu swaumu tangu kale kimekuwa kikijulikana kama 'dawa ya kushangaza' na kutumiwa na watu wengi katika kutibu mafua na influenza. Miongoni mwa faida za kitunguu swaumu ni kuzuia kupatwa na magonjwa mbalimbali na maambukizo ya virusi.

Hivyo kitunguu swaumu hujulikana kama antibiotiki ya asilia. Uchunguzi umeonyesha kwamba kula kitunguu swaumu kunapunguza kushadidi ugonjwa wa influenza na hata kuzuia kupatwa na ugonjwa huo. Vilevile kula kila mara kitunguu swaumu, huzuia kupatwa na magonjwa ya moyo, kwani kitunguu swaumu huzuia damu isigande kwenye mishipa ya damu.

Halikadhalika kitunguu swaumu ambacho pia ni kiungo muhimu cha chakula kina potassium, na hivyo watu wenye ugonjwa wa shinikizo la damu wanashauriwa kula vyakula vilivyopikwa kwa kitunguu swaumu.

Si vibaya kujua kuwa katika uchunguzi uliochapishwa mwaka 2001, imeelezwa kwamba, kitunguu swaumu kina athari kubwa na nzuri pale kinapochanganywa na baadhi ya dawa nyinginezo katika kutibu Ukimwi au HIV.

Haya shime jamani… kuanzia leo vyakula visikose kuungwa na kitunguu thomu, iwapo unaogopa kupatwa na influenza.

kwa undani zaidi gonga hapo.

http://kona-ya-afya.blogspot.com/
 
Muandishi: Othman Michuzi | Tarehe: Monday, November 23, 2009
 
Muandishi: Othman Michuzi | Tarehe: Monday, November 23, 2009
Dudu Baya akiwa na Produecer wake Juse wa huko nchini Finland
Dudu a.k.a Mamba akiwa ndani ya studio moja hivi pande za Finland
Dudu Baya akiwa kapozz na producer wake anaefahamika kwa jina la Jane,akipokuwa pande za Finland hivi karibuni.Dudu baya kwa sasa kesharejea home na baada ya kupiga bonge moja la Tour huko nchini Finland.
 
Sunday, November 22, 2009
Muandishi: Othman Michuzi | Tarehe: Sunday, November 22, 2009
Inspired by nature, the feel of the Morning Dew, The warmth of the Setting Sun, The chills of the Cool Weather,(a rarity in this Haven of Peace)…. It’s the Small things which bring Joy to Our Lives…

Mother Nature has given us in Abundance; it’s up to us how we use it as we go through this Journey called “Life”. Wastage is denying the Deprived of their Right by the Privileged Few…

“Hence Over the time since I Started My atelier we have been part of the Special Moments of So many People Lives and with each moment Came Left over Fabrics…. A pile which Kept on growing…”Hassanali Explained

The flamboyance and rich cocktail of Colour inspired this Collection of Art from Left over Fabrics and Haberdashery ranging from Khanga Kitenge, Bazein, and Satins. The Beauty of Mustafa Hassanali Signature mark to the world of Art shall bring a Different Voice that “WE CARE”

The Exhibition will run at Alliance Francaise From 23 to 28 November 2009 from 1000-1800HRS

Being Environment Conscious, Mustafa Hassanali has been selected as a Climate Change Icon by the British Council Tanzania for his role in creating an Initiative for a Better cleaner and Neater Future for Tanzanian through Art, Fashion, and Design.

Mustafa Hassanali’s commitment is to not only to promote the creative sector Industry especially Fashion in Tanzania , but also emphasise the Made in Tanzania Concept.

The Exhibition is part of Mustafa Hassanali Tenth Anniversary Celebration since His first Crowning Outfit Designed for Miss Tanzania 1999 Hoyce Temu

ABOUT MUSTAFA HASSANALI

Mustafa Hassanali is renowned for its elegance, style, flamboyancy, glamour and glitz that has made it one of the most sought after fashion houses in Tanzania

He has showcased in Africa and Europe, which has been a great influence on his approach to the world of Fashion in Tanzania . It is his exquisite handwork, detailed beadwork, and creative ensemble embellishments that make its work alive. . His showing at the Arise Africa Fashion week 2009, Durban & Cape Town Fashion Weeks, Vukani Fashion Awards in Pretoria, Miss Ethiopia Beauty Pageant, Mediterranean Fashion Festival in Sicily, Italy; M’Net Face of Africa, Mozambique, Uganda & Kenya Fashion Weeks brought him immense adulation.

His work with international Models Like Naomi Campbell, Oluchi Omweagba, Millen Magese and other International Celebrities has revolutionized the perception of the fashion scenario from Tanzania

From corporate wear, traditional costumes, or even a Wedding Ensemble, Mustafa Hassanali handles each piece with great care and gives the utmost attention to whole outfit. Each design and Outfit is Unique…. A duplicate is NEVER created.

That is what makes it uniquely, a Truly Mustafa Hassanali Affair.
Meet Mustafa Hassanali and you know what makes him special, he believes in the ‘never say die’ attitude and uses his talent and creativity in making a better today and tomorrow for the fashion fraternity along with the various social causes very close to his heart. Mustafa is truly a fashionista personified!!
 
Muandishi: Othman Michuzi | Tarehe: Sunday, November 22, 2009

 
Muandishi: Othman Michuzi | Tarehe: Sunday, November 22, 2009
magurudumu ya magari makubwa yakiwa yamehihadhiwa ili yaje kufanyiwa kazi nyingine baada ya kumaliza kazi yake ya kwanza ya kuwa kwenye magari.
 
Muandishi: Othman Michuzi | Tarehe: Sunday, November 22, 2009
kuna baadhi ya sehemu ya jiji la Dar,Network bado ni chenga kiasi kwamba ili uweze kuipata basi ni lazima upate kijisehemu kilicho juu kidogo ili uweze kuwasiliana vyema kama aonekanavyo jamaa huyu.
 
Muandishi: Othman Michuzi | Tarehe: Sunday, November 22, 2009
huku ni kama unaelekea kinondoni mkwajuni.
na huku ni kama unawelekea Magomeni morocco hotel,amba ndio kulikuwa na balaa kubwa baada ya baadhi ya daladala kuhamia upande mwingine wa barabara na kusababisha foleni kuwa kubwa.
 
Muandishi: Othman Michuzi | Tarehe: Sunday, November 22, 2009
mtaa wa congo unavyoonekana leo,hayo maji sio ya mvua bali ni chemba ambayo imejaa ndio imefanya mtaa huu kupendeza kihivi.
 
Friday, November 20, 2009
Muandishi: Othman Michuzi | Tarehe: Friday, November 20, 2009
huu ndio muonekano mpya wa barabara ya kilwa rodi kuelekea mbagala rangi tatu ambapo ndipo ulipoishia uzuri wa barabara hii,picha hii nimepiga mchana wa leo nilipokuwa naelekea kwenye mnuso huko huko mbagala.
 
Muandishi: Othman Michuzi | Tarehe: Friday, November 20, 2009
maana ngoma ndio ishakwama hapo??
 
Muandishi: Othman Michuzi | Tarehe: Friday, November 20, 2009
Bw. harusi Kassim Mussa akisikiliza kwa makini Mawaidha ya Sheikh (hayupo pichani)Bi. Shanila Zubeir akiwa katulia tulii
maharusi katika picha nzuri kabisa ya kumbukumbu.
maharusi pamoja na Mpambe wao wakielekea Nyumbani kwao. Sheikh nanihii (kati mwenye miwani) akiongozana na maharusi
"bwana Kassim Mussa,umekubali kumuona bi Sheila Zubeir kwa mahali tuliyokubaliana??"hayo ndio maneno yasemwayo hapo na kaka wa Bi. harusi.
Bw. Harusi pamoja na mpambe wake wakiwa na Sheikh aliefungisha ndoa hiyo,Sheikh Seif (kushoto) mara baada ya kumalizika kwa tendo la ufungishaji ndoa mchana wa leo maeneo ya Karakata,Tabata
Bw.Harusi na Mpambe wake wakijadili jambo
watoto wa Madrasa wakiimba qaswida katika kusherehesha harusi hiyo leo
dufu zikishughulikiwa vilivyo
kina mama wakisherehekea
msafafa umekolea,yaani simpo tu lakini ni poa

 
Muandishi: Othman Michuzi | Tarehe: Friday, November 20, 2009
Dada Alice J.B. Kibopile (Alice Ngubwene) anasikitika kutangaza kifo cha baba yake mzazi mpendwa,John Burton Kibopile wa Forest Mbeya,kilichotokea jana tar 19/11/2009 asubuhi katika hospitali ya rufaa Mbeya.
Marehemu Jonh mpaka anafariki alikuwa akisumbuliwa na ugonjwa wa shinikizo la damu na kisukari.
Aidha mazishi yamepangwa kufanyika nyumbani kwake Forest,Mbeya siku ya jumamosi (kesho) tarehe 21/11/2009.
Kwa taarifa zaidi wasiliana
na
Paul
0754294999,
Patrick
0784255413,
Alice
07i6501676/0733606
 
Muandishi: Othman Michuzi | Tarehe: Friday, November 20, 2009

SCHOLARSHIP FORUM

Napenda kuwatangazia ndugu wadau wote kuhusu maboresho niliyoweka katika mtandao kuhusiana na mambo ya scholarships. Nimeanzisha SCHOLARSHIP FORUM ambayo ni www.scholarshipnetwork.ning.com Hii ukijiunga itakusaidia kupata updates za kila scholarship info ninayoiweka katika link hiyo. Kila tangazo la scholarship niki-post hapo utapata e-mail kukujulisha.

Pia blog www.makulilo.blogspot.com nayo itaendelea kuwa hewani kama kawaida.

Mdau

MAKULILO, Jr.

San Diego, CA
 
Muandishi: Othman Michuzi | Tarehe: Friday, November 20, 2009
kondakta wa Dadadada pamoja na dereva wake wakiwa wamebeba mlango wa gari lao baada ya kudondoka wakati gari hiyo ikiwa katika mishe mishe zake za kila siku.sasa siji ingekuwa vipi kama huyo konda angening'inia mlangoni kama kawaida yao??
 
Thursday, November 19, 2009
Muandishi: Othman Michuzi | Tarehe: Thursday, November 19, 2009
What is the Kiswahili Wikipedia Challenge?

This is your opportunity to bring Africa's information online by creating Wikipedia articles in Kiswahili. You can participate by translating English Wikipedia articles into Kiswahili or by writing your own articles from scratch. You can choose your own topic to write about.

Are you a pursuing a degree in Physics?
Translate the entry for 'condensed matter' from English to Kiswahili.

Studying literature?
Write an entry on your favorite local author. Or translate an article about your favorite musician or sports team. Just think about what topics would be of interest to some of the 100 million Kiswahili speakers worldwide.

Read more about it at:
http://www.wavuti.com/4/post/2009/11
/kiswahili-wikipedia-competition.html


Subi: wavuti.com
 
Muandishi: Othman Michuzi | Tarehe: Thursday, November 19, 2009

Mtanange wa saba wa tamasha la Sauti za Busara ambalo hufanyika Zanzibar kila mwaka itakuwa ni kuanzia tarehe 11 hadi 16 Februari 2010; hakutakuwa na kiingilio kwa watakaoingia kabla ya saa kumi na moja. Sauti za Busara ni tamasha la kimataifa ambalo linautambulisha na kuutangaza muziki wa Afrika Mashariki, na ambalo hufanyika katika kila wiki ya pili ya mwezi wa Februari kila mwaka kisiwani Zanzibar.
 
Muandishi: Othman Michuzi | Tarehe: Thursday, November 19, 2009
Rais Jakaya Kikwete akiwa ameshikilia Kombe la Dunia la Mpira wa miguu baada ya kuwasili katika uwanja wa taifa Dar es Salaam. Hii ni mara ya pili kwa rais Kikwete kulibeba kombe hilo hapa nchini.
Rais Jakaya Kikwete akihutubia mamia ya wadau wa soka waliofika uwanja wa Taifa kulishuhudia kombe hilo la Dunia
Rais Jakaya Kikwete pamoja na familia yake wakipata picha ya pamoja na kombe la Dunia.picha zote na Father Kidevu Blog

HOTUBA YA RAIS WA JAMHURI YA MUUNGANO WA TANZANIA, MHESHIMIWA JAKAYA MRISHO KIKWETE KWENYE UZINDUZI WA ZIARA YA KOMBE LA FIFA LA DUNIA UWANJA WA TAIFA DAR ES SALAAM 19 NOVEMBA, 2009

Naibu Waziri wa Habari, Utamaduni na Michezo, Mheshimiwa Joel Bendera (Mb;
Mkuu wa Wilaya ya Temeke, Mhe. Chiku Garawa;
Waheshimiwa Wabunge;
Wawakilishi wa Shirikisho la Soka Duniani, FIFA;
Viongozi wa Kampuni ya Coca-Cola;
Viongozi wa Shirikisho la Soka Tanzania, TFF;
Wageni Waalikwa;Mabibi na Mabwana

Najisikia mwenye furaha kubwa kupata fursa hii ya kujumuika nanyi katika tukio hili la kihistoria kuhusu ziara ya Kombe la FIFA la Dunia hapa Tanzania.Nchi yetu imebahatika, kwa mara nyingine tena, kupata ugeni huu mkubwa wa Kombe la FIFA la Dunia ambayo ndiyo tuzo ya juu inayotolewa kwa nchi bora kuliko zote katika soka duniani. Hii ni mara ya pili sasa kwa FIFA kutupa heshima hii. Mara ya kwanza ilikuwa mwaka 2006.


Napenda kuwashukuru FIFA na Coca- Cola kwa upendeleo huo kwa nchi yetu.Kabla ya FIFA na Coca-Cola kuanzisha ziara ya Kombe la FIFA la Dunia, wapenda soka wengi duniani walikuwa wanaliona kombe hili kupitia kwenye picha za magazeti na luninga.

Leo hii kupata bahati ya kuliona kombe lenyewe “live” ni jambo la kihistoria litakalodumu katika kumbukumbu yetu kwa miaka mingi. Naipongeza FIFA kwa kuanzisha utaratibu huu wa kuwezesha maelfu ya wapenda soka duniani kuliona kombe hilo kwa karibu na wengine hata kupata nafasi ya kulishika na kupiga nalo picha.

Hii ni fursa ya pekee na ya kujivunia. Kwa Watanzania wenzangu tuichukulie ziara ya Kombe la Dunia nchini mwetu kama ni changamoto kubwa kwetu inayotutaka tufanye vizuri zaidi katika soka ili tulingane nayo heshima hii tuliyopewa.

Hasa ni changamoto kwa viongozi wa soka wa ngazi zote pamoja na wachezaji na wapenzi wa mpira wa miguu nchini. Kuja kwa kombe hili ni deni kwetu na kulilipa kwetu sisi ni kuzinduka, tuendeleze kiwango chetu cha soka nchini ili na sie siku moja tushiriki fainali za kombe hili.

Hili ni jambo linalowezekana. Wapo wenzetu Afrika wameweza, kwa nini sisi tusiweze. Wao ni watu kama sisi, maadamu wameweza na sisi tutaweza. Lakini, ili tuweze hatuna budi kuiga mfano wao hususan waliyofanya na wanayoendelea kufanya kuendeleza mpira wa miguu. Twende tukajifunze kutoka kwao.

Lakini hata kabla ya kwenda huko, yapo mambo ambayo hatuna budi kuyafanya. Naomba nitaje baadhi yake:-

1. Tuimarishe uongozi, utendaji na uendeshaji wa vilabu vya mpira. Mchezaji hufundishwa kucheza mpira katika klabu yake. Hapo ndipo hufundishwa maarifa ya kucheza mpira na vipaji kuendelezwa. Hebu tujiulize hali ya vilabu vyetu vya soka nchini ikoje.

Je vinaongozwa vizuri? Vinaendeshwa vizuri? Jibu tunalijua sote kwamba ni hapana. Lazima suala hili tulitafakari kwa yakini na kulipatia jawabu. Tukishindwa kupata jawabu muafaka na mambo yakaachwa kuendelea yalivyo, mpaka mwisho wa dunia hatutakuwa tumesogea popote.

2. Tupate walimu wenye ujuzi na uzoefu kufundisha timu zetu. Hii ndiyo njia ya uhakika ya kukuza na kuendeleza vipaji na hivyo kupata wachezaji walio bora.

3. Tuwekeze katika kuibua na kuendeleza vipaji vya wachezaji toka umri mdogo. Vilabu viwe na timu za watoto na vijana. TFF isaidie kuanzishwa kwa shule za mchezo wa mpira wa miguu kwa watoto na vijana. Mashuleni wapatikane walimu wa michezo walio wazuri kufundisha.

4. TFF ionekane zaidi ya ilivyo sasa katika mipango ya kuendeleza soka mashuleni, vijijini, mitaani na hata vilabuni. TFF ikiwa na mipango na ikasimamia na kuwabana wadau kuitekeleza itasaidia. Vinginevyo TFF itabakia kusimama ligi kuu, kutoa adhabu kwa wachezaji, na timu ya taifa.

Hiyo haitoshi.Napenda kutumia nafasi hii kutoa pongezi kwa kampuni ya Coca-Cola kwa mchango wake muhimu inaotoa kuendelea mchezo wa soka nchini na hasa soka la vijana. Mashindano ya Kombe la Copa Coca-Cola kwa vijana wa chini ya miaka 17 ni ushahidi tosha wa mchango huo adhimu.

Mashindano hayo yamegusa vijana wengi kote nchini. Naambiwa zaidi ya timu 1500 zilijitokeza kwa mwaka huu na maelfu ya vijana walijitokeza kuonyesha vipaji vyao. Naomba utaratibu huu uendelee kwani utakuwa na manufaa makubwa siku za usoni.

Maombi yangu kwa TFF ni kujipanga vizuri kutambua vijana wenye vipaji vizuri na kupanga mipango ya kuiendeleza.Ujio kwa Kombe la FIFA la Dunia hapa nchini mbali na kuhamasisha vijana wetu pia ni fursa nzuri ya kutangaza nchi yetu pamoja na fursa zake za utalii na uwekezaji.

Watu wengi zaidi wataifahamu nchi yetu vizuri zaidi kupitia ziara hii ya Kombe la Dunia. Hivi sasa tuna uwanja mpya wa kisasa ambao utaonekena vizuri wakati wa ziara hii na pengine kuvutia timu kubwa duniani kuja kufanya mazoezi hapa wakati wa fainali za Kombe la Dunia zitakazofanyika Afrika Kusini 2010.

Changamkieni fursa hii kwa maslahi ya taifa letu ili tunufaike na sisi. Baada ya kusema maneno haya machache, sasa niko tayari kufanya kazi iliyotuleta hapa sote. Nawashukuruni kwa kunisikiliza.
 
Muandishi: Othman Michuzi | Tarehe: Thursday, November 19, 2009

huyu Mama yuko pale selander brige pembeni ya kituo cha polisi cha hapo selander,kiukweli Mama huyu anasikitisha sana hasa kutokana na ile hali yake ya kufuata gari na kuomba msaada kwa alie ndani ya gari hiyo,kinachinifanya nimuonee huruma huyu Mama ni pale taa za barabara hiyo zinaporuhusu magari na yeye anapokuwa anarudi kwenye hilo baraza la katikati,yaani utamuonea huruma kwa jinsi anavyojikokota.jamani kwa nini hawa watu wanaokaa humu mabarabarani wasipatiwe msaada wa kujikwamua kimaisha na waondokane na adha hii ya kukaa sehemu kama hizi ambazo zinaweza kuhatarisha maisha yao??
 
Muandishi: Othman Michuzi | Tarehe: Thursday, November 19, 2009
 
Muandishi: Othman Michuzi | Tarehe: Thursday, November 19, 2009
hii ndio raha yake sasa,hii ni barabara ya seaview leo asubuhi
 
Muandishi: Othman Michuzi | Tarehe: Thursday, November 19, 2009
msaada hapo jamani,hivi hizo alama zinaoonekana hapo lilipopaki hilo gari na hiyo mikokoteni zinamaanisha nini??maana sisi wengine Sheria za barabarani ni ziro bin sifuri.
 
Muandishi: Othman Michuzi | Tarehe: Thursday, November 19, 2009
Meneja huduma kwa jamii wa kampuni ya simu za mikononi ya Zain Tunu Kavishe akisisitiza jambo kwa watumiaji wa mtandao wa Zain katika kilele cha tamasha la Fiesta one love.
Meneja huduma kwa jamii wa kampuni ya simu za mikononi ya Zain Tunu Kavishe akimkabidhi mtangazaji wa Clouds Fm Ephrahim Kibonde (kwa niaba ya Clouds Media Group),makao makuu ya Zain,kifurushi kama zawadi kwa ajili ya kuwapa watoto yatima na waishio katika mazingira magumu,huo ukiwa katika mchakato mzima wa kauli mbiu ya FIESTA HISANI,mchakato huo umefanyika jana ikiwa ni sehemu ya kuelekea kwenye kilele cha tamasha hilo.Kampuni ya Zain ni moja ya wadhamini wa tamasha la fiesta one love linalotarajia kufanyika keshokutwa,jumamosi katika viwanja vya posta,kijitonyama jijini Dar.
 
Idadi ya watu