Nafasi Ya Matangazo

Saturday, May 25, 2013

RAIS KIKWETE ALIPOWASILI ADDIS ABABA KUHUDHURIA SHEREHE ZA MIAKA 50 ZA UMOJA WA NCHI ZA AFRIKA (AU)

Rais Jakaya Mrisho Kikwete ni miongomi mwa marais wa bara la Afrika watakaohudhuria Sherehe za kuadhimisha miaka 50 tangu kuanzishwa kwa Umoja  wa  nchi za Afrika (AU) zinazo fanyika rasmi leo Jumamosi Mei 25, 2013 katika makao makuu ya Umoja huo jijini Addis Ababa, Ethiopia. 

 Shamrashamra zimetawala kila pembe ya jiji la Addis, wakati viongozi wa nchi za Afrika wakiwasili mmoja baada ya mwingine katika uwanja wa ndege wa kimataifa wa Bole. 

 Muungano wa Afrika wakati huo ukijulikana kama OAU, ulizaliwa Mnamo Mei 25, 1963 jijini Addis Ababa, ukianza na nchi za 32 na baadaye nchi 21 zikajiunga miaka ilivyozidi kwenda, huku Afrika ya kusini ikijiunga kuwa mwanachama wa 53 mwaka 1994. 

Mwaka 2001 OAU iligeuzwa kuwa AU katika mkutano uliofanyika Lusaka, Zambia. Jumamosi hii kutakuwa na sherehe za kilele kuadhimisha miaka hiyo 50 ya AU na kuhudhuriwa na marais karibia wote wa Afrika. 

 Kauli mbiu ya sherehe za hapo kesho ni mjadala mkuu kuhusu ushirikiano wa nchi za Afrika na kuimarishwa kwa muungano huo. Mwenyekiti wa tume ya muungano huo, Dr Nkosazana Dlamini Zuma, anaseme kuwa hii itakuwa fursa kwa AU kujadili kuhusu uwezo wa bara hili na ambacho kinaweza kufikiwa katika miaka 50 ijayo
Rais Jakaya Mrisho Kikwete akilakiwa katika Uwanja wa Ndege wa Kimataifa wa Bole jijini Addis Ababa alipowasili Ijumaa usiku  tayari kujiunga na viongozi wenzie wa nchi za Afrika katika sherehe za miaka 50  tangu kuanzishwa kwa Umoja  wa  nchi za Afrika (AU) zinazofanyika leo katika makao makuu ya umoja huo
Rais Kikwete, Mama Salma Kikwete wakiwasili Addis Ababa
Rais Kikwete na Mama Salma Kikwete wakipata maelezo ya maandalizi ya sherehe hizo toka kwa balozi wa Tanzania nchini Ethiopia, Profesa Joram Biswaro mara baada ya kuwasili Addis Ababa


DEREVA WA BODA BODA ANUSURIKA KUFA BAADA YA KUGONGWA NA LORI WAKATI AKIPITA KWENYE TAA NYEKUNDU

Lori aina ya Fuso lenye nambari za usajili T 669 CEK likiwa limeigonga pikipiki iliyokuwa inakatiza kwenye taa nyekundu mapema leo katika eneo la Majumba sita njia panda ya Segerea.Waendesha pikipiki wengi wamekuwa wakiuendeleza uzembe huu ambao umekuwa ukifumbiwa macho sana na Watu wa Usalama Barabarani.
Huyu ndie dereva wa pikipiki hiyo akiugulia maumivu kabla ya kupatiwa msaada wa kukimbizwa hospitali.Picha na Adam Mzee.


Warembo wa Kigamboni wapewa Somo na Miss Tanzania wa Zamani

Warembo wa Miss Kigamboni 2013 wakipewa somo na Miss Tanzania mwaka 1999,Hoyce Temu wakati alipowatembelea kwenye kambi yao kwa lengo la kuwafunda warembo hao,Hoyce aliwaaambia warembo hao mambo mbali mbali kuhusiana na masuala ya urembo likiwemo suala la nidhamu na kujitambua katika jamiii. Shindano la miss kigamboni litafnyika juni 7 mwaka huu,huko Kigamboni jijini Dar.
Miss Tanzania mwaka 1999,Hoyce Temu (wa pili kushoto) akiwa kwenye picha ya pamoja na Warembo wa Miss Kigamboni 2013.


Wabunge wanawake wajinoa kuhusu namna bora ya uwasilishaji wa Miswada na Hoja Binafisi Bungeni

Chama cha Wabunge wanawake katika Bunge la Tanzania (TWGP) leo wamefanya semina ya siku moja kwa wabunge wote wanawake kwa lengo la kuongeza uelewa mpana katika namna bora ya uwasilishaji Miswada au hoja binafsi Bungeni.

Akifungua semina hiyo, Mwenyekiti wa chama hicho cha Wabunge wanawake Bungeni. Mhe. Anna Abdallah amewataka wabunge wanawake wote bila kujali vyama vyao kuhakikisha wanaitumia vizuri Ofisi ya mshauri mkuu wa mambo ya sheria wa Bunge katika kuwasilisha Miswada au hoja Binafisi.

Amesema wabunge wanawake wanawajibu wa kutatua matatizo yanayowakabili wananchi hususani wanawake nchini ikiwa ni pamoja na kuleta hoja au miswada Bungeni yenye kulenga kuifanya serikali iweze kutatua kero zinazowakabili wananchi wake.

“Waheshimiwa wabunge, pamoja na kwamba mimi nikipindi changu cha nane hivi sasa bado kuna mwamko mdogo kwa waheshimiwa wabunge wanawake kuleta miswada au hoja binafsi bungeni. Naamini tukiitumia vizuri Ofisi hii pale tutakapokuwa tuna mawazo yetu, watatusaidia sana kutuandalia hoja binafisi au miswada kulingana na matakwa yaliyopo ya kikanuni”alisema Mhe. Anna Abdallah

wakichangia mada zilizowasilishwa hapo, wabunge wengi wanawake wameomba kuwe na utaratibu mzuri wa kuhakikisha kuwa kila mara elimu hii inatolewa kwa lengo la kujikumbusha baadhi ya taratibu za kikanuni na hata kisheria katika uwasilishaji wa hoja binafsi na miswada binafsi Bungeni.

“Kuna haja ya kuwa na semina katika maswala haya angalau mara moja kila wakati wa vikao vya Bunge ili kujikumbusha mambo kadhaa yanayotawala katika uwasilishwaji wa miswada binafsi au hoja Binafsi mwenyekiti kwa kuwa tuna mambo mengi tungependa kuyaleta Bungeni kupata baraka zake. Kwa kujikumbusha na mambo haya tutaiva kwelikweli katika kuwawakilisha wananchi wetu mwenyekiti”. Alichangia Mhe. Anne Kilango Malecela.

Jumla ya mada tatu ziliwasilishwa katika Semina hiyo iliyoandaliwa na chama hicho cha wabunge wanawake Bungeni (TWGP) kwa kushirikiana na Ofisi ya msahuri wa maswala ya sheria wa Bunge ambazo zote zililenga kuwapa uelewa wabunge kuhusu namna bora na mambo ya kuzingatia wakati wa kuwasilisha miswada binafsi na hoja binafsi Bungeni kwa wabunge wanawake.
Mwenyekiti wa Chama cha Wabunge wanawake Bungeni (TWGP) . Mhe. Anna Abdallah (Mb) akifungua rasmi semina hiyo siku moja kuhusu namna bora ya uwasilishaji wa Miswada binafsi na hoja Binafisi Bungeni kwa wabunge wanawake. Kushoto ni katibu wa chama hicho Mhe. Angela kairuki na aliyekulia ni Makamu Mwenyekiti Mhe. Dkt. Mary Mwanjelwa.
Mtoa mada kutoka Ofisi ya Mshauri Mkuu wa mambo ya Sheria wa Bunge Ndg. Matamusi Fungo akiwasilisha mada kwa wabunge wanawake kuhusu uwasilishwaji wa Miswada ya Serikali Bungeni.
Bi. Stella Bwimbo nae kutoka Ofisi ya Mshauri Mkuu wa mambo ya Sheria wa Bunge akiwasilisha mada kuhusu uwasilishwaji wa Miswada binafsi ya sheria Bungeni.
Ndg. Mosi Lukuvi kutoka Ofisi ya Mshauri Mkuu wa mambo ya Sheria wa Bunge akiwasilisha mada kuhusu uwasilishwaji wa Hoja binafsi Bungeni kwa waheshimiwa wabunge wanawake.
Katibu wa Chama cha Wabunge wanawake Bungeni Mhe. Angela kairuki akikaribisha michango kwa waheshimiwa wabunge mara baada ya kusikiliza mada. Kushoto ni Makamu Mwenyekiti wa chama hicho Mhe. Dkt. Mary Mwanjelwa.
Mbunge wa Same Mashariki Mhe. Anne Kilango Malecela akichangia mada wakati wa semina hiyo.
Mbunge wa viti Maalum (CCM) Diana Chilolo akiuliza swali kwa mtoa mada.
Mbunge wa Viti Maalum (CHADEMA) Mhe. Cecilia Paresso akiuliza swali kwa watoa mada.
Mbunge wa viti Maalum (CCM) Devota Likokola nae akichangia.
Mbunge wa viti Maalum (CCM) Maria Hewa akitoa mawazo yake.


WATAALAM WA TIBA ZA ASILI NA TIBA MBADALA WAKUTANA JIJINI DAR ES SALAAM

Kaimu mganga mkuu wa serikali Dkt. Mohamed Mohamed akifungua mkutano wa Baraza la wataalam wa Tiba za Asili na Tiba mbadala leo jijini Dar es salaam waliokutana kujadili mafanikio, changamoto na mipango mbalimbali waliyonayo katika utoaji wa huduma bora za afya kwa wananchi.
Kaimu Mkurugenzi wa Masuala ya Tiba za Asili na Tiba Mbadala wa Wizara ya Afya na Ustawi wa Jamii Dkt.Paulo Mohammed akitoa ufafanuzi wa hali halisi ya Tiba za Asili na Tiba mbadala nchini Tanzania na mpango wa serikali wa kuendelea kuthamini huduma inayotolewa na wataalam hao wakati wa mkutano wa Baraza la wataalam wa Tiba za Asili na Tiba mbadala.
Mratibu wa Tiba za Asili na Tiba Mbadala kutoka Shirika la Afya Duniani (WHO) Rose Shija akisoma salam za mwakilishi wa Shirika la Afya Duniani nchini Tanzania Dkt. Rufaro Chatora leo jijini Dar es salaam ambaye amepongeza juhudi zinazofanywa na serikali ya Tanzania kupitia Wizara ya Afya kutatua changamoto zinazowakabili wataalam wa Tiba za Asili na Tiba mbadala.
Mtafiti mwandamizi mkuu wa Idara ya Utafiti wa Tiba Asili kutoka Taasisi ya Utafiti wa magonjwa ya Binadamu Hamis Masanja Malebo akitoa mada kuhusu historia ya Tiba za Asili na uhusiano uliopo katika matumizi ya mimea ya asili kati ya tiba za asili na tiba mbadala na tiba za kisasa katika utengenezaji wa dawa. Picha na Aron Msigwa - MAELEZO.
Sehemu ya wataalam wa Tiba za Asili na Tiba mbadala waliohudhuria mkutano wa Baraza la Wataalam wa tiba hiyo wakifuatilia masuala mbalimbali wakati wa mkutano huo leo jijini Dar es salaam. Picha na Aron Msigwa - MAELEZO.


Friday, May 24, 2013

ANAEDAIWA KUCHOCHEA VURUGU NA FUJO NCHINI AKAMATWA

Jeshi la Polisi Nchini linamshikilia mtu mmoja ambaye jina lake linahifadhiwa kwa sababu za kiupelelezi kwa tuhuma za kueneza ujumbe wa uchochezi na chuki kwa wananchi na viongozi wa serikali kwa njia ya simu ya mkononi akituma SMS kwa lengo la kuchochea fujo, vurugu na kutoa matusi kwa viongozi hao.

Mtu huyo amekuwa akifanikisha kazi hiyo kwa kutumia Chips (sim card) 13 za simu za mkononi ambazo amekamatwa nazo. Jeshi la Polisi linaendelea kumhoji mtu huyo na ushahidi utakapokamilika atafikishwa mahakamani.

Aidha, Jeshi la Polisi linatoa wito kwa wananchi wenye taarifa zingine za wahahlifu kama hao kujitokeza na kutoa taarifa hizo polisi ili wahalifu hao waweze kukamatwa na kuchukuliwa hatua stahiki, wakiwemo watu wanaowashawishi wenzao kwa njia ya fedha, kuwashauri ama kuwasaidia kwa namna yeyote ile katika kufanikisha uhalifu huo na kusababisha uvunjifu wa amani hapa nchini. Jeshi la polisi halitasita kumchukulia hatua mtu yeyote atakayebainika kuvunja sheria za nchi.

Imetolewa na:-
Advera Senso-SSP
Msemaji wa Jeshi la Polisi.


RAIS JAKAYA KIKWETE AFUNGUA MAONYESHO YA MFUMO WA MATOKEO MAKUBWA 'SASA' AWAMU YA KWANZA

Rais Jakaya Kikwete, Makamu wake Dkt. Mohammed Gharib Bilal na Waziri Mkuu, Mizengo Pinda, wakiwasili kwenye Ukumbi wa Jumba la Makumbusho ya Taifa, leo Mei 24, 2013 kwa ajili ya Kufungua rasmi Maonesho ya Mfumo wa Matokeo Makubwa 'Sasa' Awamu ya kwanza.
Rais Jakaya Kikwete, Makamu wake Dkt. Mohammed Gharib Bilal na Waziri Mkuu, Mizengo Pinda, wakisikiliza maelezo kutoka kwa Mchambuzi Sera Mkuu wa Ofisi ya Rais na Mipango, Lorah Madete, wakati walipokuwa wakitembelea Maonesho ya Mfumo wa Matokeo Makubwa Sasa Awamu ya Kwanza, baada ya kuyafungua rasmi leo katika Ukumbi wa Makumbusho ya Taifa, Jijini Dar es Salaam.
Rais Jakaya Kikwete, Makamu wake Dkt. Mohammed Gharib Bilal na Waziri Mkuu, Mizengo Pinda, wakisikiliza maelezo kutoka kwa Ofisa Mtafiti Mkuu wa Wizara ya Kilimo, Dkt. Mary Shetto, wakati walipokuwa wakitembelea Maonesho ya Mfumo wa Matokeo Makubwa Sasa Awamu ya Kwanza, baada ya kuyafungua rasmi leo katika Ukumbi wa Makumbusho ya Taifa, Jijini Dar es Salaam.
Rais Jakaya Kikwete, Makamu wake Dkt. Mohammed Gharib Bilal na Waziri Mkuu, Mizengo Pinda, wakiwa kwenye Ukumbi wa Makumbusho ya Taifa wakati wa Ufunguzi rasmi wa Maonesho ya Mfumo wa Matokeo Makubwa 'Sasa' Awamu ya Kwanza leo Mei 24, 2013.
Msanii maarufu wa kughani, Mrisho Mpoto, wakibinjuka Sarakasi, wakati kikundi chake na Bendi yake ya Mjomba ilipokuwa ikitoa burudani katika Maonesho ya Mfumo wa Matokeo Makubwa 'Sasa' Awamu ya Kwanza, yaliyofunguliwa na Rais Jakaya Kikwete, leo Mei 24, 2013.
Wanamuziki wa Bendi ya Mjomba, wakiimba kutoa burudani katika Maonesho ya Mfumo wa Matokeo Makubwa 'Sasa' Awamu ya Kwanza, yaliyofunguliwa na Rais Jakaya Kikwete, leo Mei 24, 2013. Picha na OMR


UJUMBE MUHIMU

Katika barabara mbali mbali hapa nchini hasa katika maeneo yale yenye madaraja,kumekuwa na vibao vya tahadhali kama hivyo kionekanacho pichani hapo,ili kufanya barabara zetu ziendelee kuwa imara.kibao hilo kipo katika barabara mpya ya kutoka Bagamoyo mpaka Msata.


HAKUNA JAMII ITAKAYOACHWA NYUMA KIMAENDELEO-TANZANIA


Balozi Ramadhan Mwinyi Naibu Mwakilishi wa Kudumu wa Tanzania katika Umoja wa Mataifa, akizungumza wakati wa Mkutano wa Kudumu wa 12 wa Masuala ya Wazawa, katika mchango wake kuhusu mada ya utafiti uliofanywa kuhusu Ujasiri, Maarifa ya Jadi na Kujenga uwezo Jamii ya Wafugaji katika Afrika, Mwakilishi huyo ameeleza kwamba Jamhuri ya Muungano inajukumu la kuwaletea maendeleo wananchi wake wote na kwamba katika hakuna jamii itakayoachwa nyuma. Akasisitiza haja na umuhimu wa Jumuiya ya Kimataifa na wadau wengine kushirikiana na Serikali kufanikisha azma hiyo lakini pia kuunga mkono hatua na maamuzi inayoyachukua kwa manufaa ya wananchi wake na taifa kwa ujumla. Nyuma ya Balozi ni Bi. Ellen Maduhu Afisa wa Ubalozi .

Na Mwandishi Maalum

 Jamhuri ya Muungano wa Tanzania imesisitiza kwamba inajukumu kubwa  la kuhakikisha kuwa mipango yake ya maendeleo endelevu inamfikia kila mwananchi na kwamba hakuna jamii itakayo achwa nyuma.
Na kwa sababu hiyo, Tanzania imeitaka  Jumuiya ya Kimataifa na wadau wengine kushirikiana na Serikali katika kufanikisha azma  yake hiyo, lakini pia kutambua  kuwa maamuzi mbalimbali inayoyachukua  yanafanyika kwa nia njema.

Hayo yameelezwa na   Balozi  Ramadhan Mwinyi, Naibu Mwakilishi wa Kudumu wa   Tanzania katika Umoja wa Mataifa,  alipokuwa akichangia  majadiliano ya mada   ya utafiti kuhusu Ujasiri, Maarifa ya Jadi na Kujenga Uwezo wa Jamii ya  Wafugaji katika Afrika.

Mada  hiyo ni sehemu ya mada kadhaa zikiwa zao afya, elimu, haki za binadamu, ujasiliamali, vijana mila na tamadu ambazo zimekuwa zikijadiliwa kwa nyakati tofauti katika Mkutano wa Kudumu wa 12  Kuhusu Masuala ya Wazawa. ( Forum on Indigenous Issues) Mkutano huu ambao ulianza mapema wiki hii unafanyika chini ya  usimamizi wa  Baraza la Uchumi na Maendeleo ya Jamii la Umoja wa Mataifa ( ECOSOC).

Washiriki wa  mkutano  huu wapatao 2000 wanatoka katika Asasi zisizo za kiserikali  wakiwamo wawakilishi kutoka   baadhi ya  taasisi za kifedha kama  Banki ya Dunia,  Banki ya Maendeleo ya Afrika  na  Banki  ya Maendeleo ya Asia.

“Tunaendelea na  jitihada za kuwaletea maendeleo wananchi wetu ili kuhakikisha kwamba hakuna jamii inayoachwa nyuma kama ambavyo imeainishwa katika Malengo ya Maendeleo ya Millenia ( MDGs) na  kutafsriwa katika Mpango wa Maendeleo ya Taifa na  mipango migineyo” akasisitiza Balozi Mwinyi.

Hata hivyo akasema licha ya jitihada hizo za serikali , bado kuna baadhi ya jamii chache ambazo zenyewe zimeamua    kudumisha  mila, tamaduni na   maisha yao ya jadi .

Akasema  jamii hizo ni zile ambazo hazifahamiki sana katika Jumuiya ya Kimataifa kama ilivyo kwa jamii ya  wamasaai.

Akizungumzia  masuala ya upatikanaji na ugawaji wa ardhi kwa wananchi  zikiwamo  jamii ambazo mfumo wa maisha yao unategemea zaidi ardhi na mali asili nyingine. Balozi   Mwinyi amewaeleza washiriki  wa  mkutano huo wakiwamo washiriki kutoka Tanzania, kwamba serikali imejiwekea sheria na taratibu zinazosimamia ugawaji wa ardhi.

Akafafanua  kwa kueleza kwamba kwa sheria na taratibu za Tanzania,   Hati ya umiliki wa Ardhi katika  ngazi ya kijiji hutolewa  kwa wanajamii ambao wanaishi au wamekusanyika katika  muundo wa kijiji ambao unatambuliwa rasmi.

“ Kwa mujibu wa sheria zetu, ni kijiji ndicho kinatambuliwa kisheria  kama chombo huru kinachosimamia masuala ya ardhi ambapo cheti  cha ardhi hutolewa kwaajili ya matumizi ya jamii nzima”. Akasema
Na kuongea “ Hata hivyo    kuna  baadhi ya maeneo  hasa yale ya wawindaji ambapo kama idadi ya  jamii ile haikukidhi  matakwa ya kisheria ya kuwa na hadhi ya kijiji kutokana na uchache wao, bado kwa mfano,  mwaka 2011, serikali ilitoa  hati ya  kumiliki ardhi kwa ya Wahdzabe ingawa walikosa sifa  zinazotakiwa kisheria.

Akizungumza kuhusu  Loliondo ambako  Serikali imetangaza kutenga eneo la kiasi cha kilomita za mraba 2,500  za ardhi kwaajili ya  makazi ya jamii ya wamasaai  na ambao wengi wao hawakuwa na ardhi na hivyo kuwa katika mazingira magumu. Balozi amesisitiza kwamba uamuzi huo ulikuwa ni wa manufaa kwa jamii hiyo na taifa kwa ujumla.

Akasema kuwa  eneo  lililotengwa   ni kubwa  kuliko nchi ya Luxeburg au  mara nne ya eneo la nchi ya Singapore ambayo ina kilomita za mraba 624.

Akasema eneo  lililobaki la kilomita za mraba 1,500 Serikali imelitenga kwaajili ya hifadhi ya wanyama pori na mazalia yake ikiwa ni  pamoja na uhifadhi wa uoto wa asili, utunzaji wa vyanzo vya maji  kwa maendeleo endelevu ya  uwepo wa wanyama na kwa manufaa ya vizazi vya sasa na vijavyo.

Naibu Mwakilishi wa Kudumu akafafanua Zaidi kwa kueleza kwamba, uamuzi huu wa Serikali wa kutenga ardhi kwaajili ya matumizi ya binadamu na mengine  kwa hifadhi ya  maliasili ni uamuzi halali na wala haukuanza sasa  bali umekuwa  ukitekelezwa katika  maeneo mengi ya nchi tangu uhuru.


NSSF YAWAPOKEA WANACHAMA WAPYA WA HIARI 500 JIJINI TANGA

Mkuu wa Wilaya ya Mkinga Bi Mboni Mgaza akiwasalimia wakazi wa Kata ya Kwale, Wilayani Mkinga ambapo zaidi ya Wananchi Mia Tano (500) wamejiunga na NSSF kama wanachama wa hiari.
Mkurugenzi wa Uendeshaji wa NSSF Bw. Crescentius Magori akisoma hotuba kwa niaba ya Mkurugenzi Mkuu wa NSSF. Kushoto kwake ni Mkuu wa Wilaya ya Mkinga Bi Mboni Mgaza na Meneja Wa NSSF mkoa wa Tanga Bw. Frank Maduga. Kulia kwake Ni Bi Eunice Chiume, Meneja Kiongozi wa Uhusiano na Uhuduma kwa Wateja.
Mwenyekiti wa Kijiji cha Kichalikani akimkabidhi Mkuu wa Wilaya ya Mkinga Bi Mboni Mgaza hotuba ya wakazi wa Kata ya Kwale.
Mkuu wa Wilaya ya Mkinga Bi Mboni Mgaza akiwakabidhi wanachama wapya wa hiari wa NSSF katika Kata ya Kwale.
Bango la kuwakaribisha wavuvi wa Kata ya Kwale, kijiji cha Kichalikani kujiunga na Mfuko wa Taifa wa Hifadhi ya Jamii (NSSF) kama wanchama wa Hiyari.


MRADI WA UENDELEZAJI MIJI TANZANIA (TSCP) WAENDELEA KWA KASI

Timu ya wataalamu kutoka OWM-TAMISEMI-katika Mradi wa Mpango Miji Mkakati (TSCP ) Pamoja na wawakilishi kutoka Benki ya Dunia pamoja na Ubalozi wa Denmak wakikagua Ujenzi wa Barabara zinazoendelea kujengwa kupitia mradi wa TSCP katika Mnispaa ya Mtwara Mikindani katika kubaini utekelezaji na maendeleo ya maeneo mbalimbali ya mradi.
Wafanyakazi wa TSCP na Mwakilishi wa Benk ya Dunia wa kwanza kulia wakifuatilia kwa makini uwasilishwaji wa maendeleo ya Mradi wa TSCP katka Mnispaa ya Mtwara Mikindani katika kubaini utekelezaji na maendeleo ya maeneo mbalimbali ya mradi.
Ujenzi wa kituo cha basi cha kigoma ujiji ukiendelea.


Toka uzinduzi wa mradi wa uendelezaji Miji. Tanzania Strategic Cities Project (TSCP), mnamo mwaka 2010. Mradi umekuwa ukiboresha huduma za msingi mijini kufikia walengwa. Mradi huu wa uendelezaji miji Tanzania umeundwa kwa ajili ya kukabili changamoto mbalimbali za Miji ya Tanzania. Mradi huu unatekelezwa na Halmashauri nchini, chini ya usimamizi wa Ofisi ya Waziri Mkuu – Tamisemi. 

Mradi huu ni mkopo kutoka Benki ya Dunia na ruzuku kutoka Danida. Mwanzoni mwa wiki mwandishi wetu aliongea na Kaimu Katibu Mkuu wa Tamisemi Bwn. Jumanne Sagini ambaye alikua na haya ya kusema “Mradi wa uendelezaji miji Tanzania upo na una lengo la kuboresha viwango na kurahisisha ufikiwaji wa huduma za msingi Mijini kwa kukarabati na kupanua miundombinu ya Miji pamoja na kuziimarishia uwezo taasisi husika katika kuboresha mapato na usimamizi wake” Bwn. Jumanne Sagini aliendelea kusema “Mradi huu umegawanyika katika maeneo makuu matatu ambayo ni Miundo mbinu na huduma za miji; 

Uimarishaji wa Taasisi pamoja na Usimamizi wa Mradi; na ni miji saba tu ndiyo itakayofaidika na mradi huu. Miji yenyewe ni Tanga, Arusha, Mwanza, Kigoma, Mbeya, Mtwara, na Dodoma, Kwa Mji wa Dodoma, Mradi unatekelezwa na Halmashauri ya Manispaa Dodoma Ustawishaji Makao Makuu Dodoma (CDA)”. 

Mradi huu unagharama ya $ 175.5, ambapo $162.8 ni mkopo kutoka Benki ya Dunia na $12.7 ni ruzuku kutoka DANIDA. Mkopo wa Benki ya Dunia ni kwa ajili ya maeneo ya Miundombinu na huduma za miji, wakati ruzuku kutoka DANIDA itagharamia uimarishaji wa Taasisi katika kutekeleza majukumu yake. Ili kujua kwa undani zaidi kuhusu mradi huu, Mwandishi wetu wa habari aliongea na Mratibu wa mradi huu Mhandisi Davis Ben Shemangale. Mhandisi Davis Ben Shemangale alielezea 

 “Mradi huu ni njia ya kutekeleza dhana ya kugatua madaraka toka Serikali Kuu kwenda kwa umma, mradi huu wa TSCP unaendeshwa na Halmashauri husika kwa kuchagua na kuitekeleza miradi kwa kadri ya vipaumbele vyao”. 

Mhandisi Davis Ben Shemangale alimalizia kwa kusema “mradi huu umewekwa katika awamu tatu hadi nne kwa kila mji na mpaka sasa wakandarasi kwa awamu zote wamekwisha anza kazi” aliendelea kwa kusema “wakandarasi kwaajili ya kutekeleza awamu ya kwanza walianza kazi Novemba mwaka 2011 na awamu ya pili walianza kazi mwezi June mwaka 2012 ambapo awamu ya tatu na ya nne walianza kazi mwezi Novemba 2012”


 
Modified by MKCT
Idadi ya watu
Idadi ya watu